TPDC kujenga kiwanda Lindi
Shirika
la Maendeleo ya Petroli Nchini -TPDC kwa kushirikiana na kampuni za
kimataifa za mafuta inatarajia kujenga kiwanda cha kuchakata gesi asilia
LNG katika eneo la Likong’o katika Manispaa ya Lindi
Akifungua mkutano wa wadau wa gesi na kampuni za utafiti
wa gesi jijini Dar Es Salaam Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na
Madini Profesa James Mdoe amesema kiwanda hicho kitaifanya gesi kuwa
kimiminika na kuwekwa katika mitungi kwa ajili ya matumizi ya majumbani
na viwandani.Naye Mkurugenzi wa utafiti wa gesi mkondo wa chini wa TPDC, Kelvin Komba amesema kazi ya ujenzi wa kiwanda hicho utaanza baada ya taratibu za kimikataba kukamilika.
Egidius Audax
No comments