Swissport kujenga bohari
Kampuni
ya upakuaji na upakiaji mizigo kwenye ndege ya Swissport Tanzania
imewekeza shilingi bilioni 26 kujenga bohari ya kisasa ya mizigo katika
uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar Es
Salaam
Swissport kujenga bohari
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa jengo hilo, Afisa
Mtendaji Mkuu wa kampuni hiyo Gaudence Temu amesema bohari hiyo ina
mitambo ya baridi ya kuhifadhi mizigo inayoharibika haraka, mitambo ya
ukaguzi, mizani, vyumba vya kuhifadhia wanyama wadogo na mizigo ya
kawaida.Katika hatua nyingine Mkurugenzi wa Fedha wa kampuni hiyo Mrisho Yasini amesema Swissport imepata tuzo ya kimataifa inayotambuliwa na Shirikisho la Usafiri wa Kimataifa wa Anga ya ISAGO kwa kutambua huduma bora inazozitoa kwa abiria wa ndege na mizigo yao.
Stanley Ganzel
No comments