Polisi waua mtu anayesadikiwa kuwa jambazi Kagera
Vitendo
vya utekaji na uporaji wa mashine za mitumbwi na mali nyingine katika
baadhi ya visiwa vilivyopo ndani ya ziwa Victoria mkoani Kagera
Katika tukio la hivi karibuni mtu mmoja anayesadikiwa kuwa ni jambazi ameuawa wakati wa mapambano ya kurushiana risasi baina ya Polisi na majambazi waliovamia kisiwa cha Mazinga wilayani Muleba na kupora mashine na mtumbwi uliokuwa na samaki.
Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Kagera Augustino Ollomi amesema katika mapambano hayo ya kurushiana risasi yaliyoendelea hadi katika kisiwa cha Ghana karibu na wilaya ya Ukerewe mkoani Mwanza, mtu mmoja anayesadikiwa kuwa jambazi aliuawa huku mwenzake mmoja akijisalimisha.
Kamanda huyo wa Polisi wa mkoa wa Kagera amehimiza dhana ya ulinzi shirikishi katika visiwa hivyo.
Charles Mwebeya
No comments