• Breaking News

    Rais Mstaafu Kikwete atembelea daraja la Nyerere


    Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Rais mstaafu Jakaya Kikwete ametembelea daraja la Nyerere lililoko jijini Dar Es Salaam
    Mwenyekiti wa CCM, Rais Mstaafu Jakaya Kikwete na Mama salma Kikwete wakitembea kwenye daraja hilo leo. Kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda
    Mara baada ya kuangalia maeneo kadhaa ya daraja hilo, Dkt. Kikwete amekuwa na kikao cha faragha na baadhi ya watendaji wa mkoa wa Dar Es Salaam na Mfuko wa Taifa wa  Hifadhi ya Jamii -NSSF kujadili mikakati mbalimbali ya kutunza daraja hilo.

    Kando ya ziara hiyo Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi Joseph Nyamhanga ametangaza rasmi tozo kwa vyombo vya usafiri vitakavyopita kwenye daraja la Nyerere lililopo jijini Dar Es Salaam.

    Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya ziara ya Rais Mstaafu wa awamu ya Nne Dkt. Jakaya Kikwete iliyokua na lengo la kuangalia daraja hilo, Nyamhanga amesema tozo hizo zitatofautiana kulingana na ukubwa wa chombo husika.

    Mkurugenzi wa uwekezaji kutoka NSSF, Yacoub Kidula amesema tozo hizo zitaanza kutumika rasmi tarehe 14 mwezi huu.

    Norah Uledi

    No comments

    Post Top Ad