Bandari ya TANGA yashinda zabuni ya kujenga bomba la mafuta
Waziri
wa Nishati na Madini Profesa SOSPETER MUHONGO amesema bandari ya TANGA
imeshinda zabuni ya ujenzi wa bomba la mafuta Kutoka Ziwa ALBERT nchini
Uganda
Waziri wa Nishati na Madini Profesa SOSPETER MUHONGO amesema
bandari ya TANGA imeshinda zabuni ya ujenzi wa bomba la mafuta Kutoka
Ziwa ALBERT nchini Uganda hadi bandari ya TANGA kutokana na kigezo cha
kuwa na kina kirefu na mazingira ya kijiografia ambayo yanaiwezesha
kustahimili mawimbi makali ya bahari.
Akizungumzia ushindi huo ametaja sababu nyingine ya Tanzania kuchaguliwa katika mradi huo wa bomba la mafuta kuwa ni njia ambayo bomba hilo litapita ni ya mteremko hali itakayosaidia kupunguza gharama za kupampu mafuta.
Aidha sababu zingine ni usalama wa Tanzania ukilinganisha na nchi kama KENYA iliyokumbwa na matukio ya ugaidi pamoja na uzoefu mkubwa katika uendeshaji wa mabomba ya mafuta kama lile la TAZAMA.
MUHONGO ameainisha baadhi ya faida ambazo Tanzania itazipata ni ajira kwa vijana.
April 25, 2016
DOMINIC MOKIWA
Akizungumzia ushindi huo ametaja sababu nyingine ya Tanzania kuchaguliwa katika mradi huo wa bomba la mafuta kuwa ni njia ambayo bomba hilo litapita ni ya mteremko hali itakayosaidia kupunguza gharama za kupampu mafuta.
Aidha sababu zingine ni usalama wa Tanzania ukilinganisha na nchi kama KENYA iliyokumbwa na matukio ya ugaidi pamoja na uzoefu mkubwa katika uendeshaji wa mabomba ya mafuta kama lile la TAZAMA.
MUHONGO ameainisha baadhi ya faida ambazo Tanzania itazipata ni ajira kwa vijana.
April 25, 2016
DOMINIC MOKIWA
No comments