• Breaking News

    RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 79 & 80 (Riwaya inawafaa kuanzia miaka 18 na kuendelea )

    Mtunzi : Eddazaria g.Msulwa

    ILIPOISHIA
    Gari nne nyeusi, zenye muundo wa gari kama zinazo bebea pesa za mabenki, zikafunga breki katika eneo tulilopo. Wakashuka watu walio valia ñguo nyeusi, makofia meusi yaliyo waficha sura zao, na kubakishs macho yao tu. Kila mmoja mkononi mwake ameshika bundiki, na wote wakanizungu huku wakinitazama kwa umakini.

    ENDELEA
       Mmmoja wao akatoa amri ya mimi kuiamsha mikono yangu juu, nikatii pasipo kubishana. Akatoa amri nyingine ya mimi kulala chini, hapo ndipo nilipo anza kuleta ubishi, kwani siwezi kukamatika kirahisi.

    Kitendo cha mimi kusogeza mguu nyuma, nikastukia kitu chenye ncha kali kikinichoma mgongoni, kwa haraka nikaupeleka mkono wangu nyuma, kwa ajili ya kukichomoa. Nikakuta ni sindano
    yenye dawa, iliyo anza kuvinyong'onyeza viungo vyangu vya mwili. Taratibunikajikuta nikianza kuishiwa na nguvu. Nikaanguka chini, kila nilipo jaribu kunyanyua hata mkono sikuweza, nikajikuta nikiwatazama watu hao walio nikaribia na kuninyanyua. Nikastukia kitu kizito kikinipiga, kichwani, giza kali likanitawala machoni mwangu.

                ********
    "Eddy.... Eddy"
    Nisauti nyororo, iliyo anza kuisikia taratibu, ikipenya masikioni mwangu. Taratibu nikayafungua macho yangi, nikakutana na sura ya kike, huku kichwa chache kikiwa kimejaa nywele nyingi nyeusi na zilizo ndefu sana.

    Macho yake makubwa kiasi, na yadura kiasi, yaliendelea kunitazama huku akiwa ameniimamia, kutoka katika kitanda nilicho kilala.
    "Karibu tena duniani" Alizungumza huku akiwa ametabasamu.
    "Duniani?"
    "Ndio duniani"
    "Kwani nilikua, sipo duniani?"
    Hakuzungumza chochote zaidi ya kusimama, pembeni ya kitanda nilicho lala.
    "Kwa jina ninaitwa dokta, Agines, nimtaalamu katika maswala ya saikolojia"
    "Ngoja, hapa ni wapi?"
    "Upo Washinton DC, Marekani"
    "Ahaaaa?"
    "Usishangae, ninaimani kwamna unatambua, nitukio gani ulilo lifanya kwa ajili ya hii nchi, nasi tumeamua kukuweka karibu nasi na kukusaidia kwa kila jambo"

     Akafungua pazia, kubwa lililopo kwenye moja ya ukuta, hapa ndipo nilipo anza kuona majengo makubwa yaliyopo katika mji huu, ambapo ndipo yalipo makao makuu ya serikali ya nchi ya Marekani.
    "Tutahakikisha tunakufanyia kila unacho kihitaji"
    Akaniandalia chakula, akaniomba nile.
    "Ukimaliza kula, kuna watu nitahitaji uonane nao"
    "Wakina nani?"
    "Utawaona tuu"
    Nikamaliza kula, akanionyesha bafuni, nikaoga na kurudi kitandani, huku nikiwa nimejifunga taulo.
    "Unaweza kuvaa"
    "Mbele yako?"
    "Kwani kuna tatizo lolote, tambua kwamba mimi nitakuwa pamoja nawe kwakipindi cha siku tisini"
    "Za nini?"

    "Eddy vaa bwana, watu hao wanakusubiri."
    Nikamtazama kwa muda, nikavua taulo, nikachukua nguo moja baada ya nyingine alizo zipanga kwenye kitanda.
    "Umependeza sana"
    "Asante"
    "Upo tayari"
    "Ndio"

    No comments

    Post Top Ad