Mkwasa azungumzia AFCON
Kocha
Mkuu wa timu ya soka ya Tanzania, Charles Mkwasa amesema mchezo dhidi
ya Misri utakuwa ni fainali ya kuamua taifa litakalofuzu kucheza katika
fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika -AFCON mwakani kutoka kundi G
Kocha Mkuu wa timu ya soka ya Tanzania, Charles Mkwasa
Mkwasa amesema Misri wanahitaji sare ili wafuzu kwa fainali hizo, lakini hawataipata kupitia mgongo wa Taifa Stars.
Misri inaongoza kundi G ikiwa na alama saba, ikifuatiwa na Nigeria wenye alama mbili huku Taifa Stars ikiwa na alama moja na hivyo inahitaji kuifunga Misri ili kufufua matumaini ya kufuzu kwa fainali hizo za AFCON.
Taifa Stars itamaliza mechi zake za kufuzu kwa fainali za AFCON 2017 kwa kucheza na Nigeria mwezi September mwaka huu mjini Abuja.
CHANZO:TBC
Misri inaongoza kundi G ikiwa na alama saba, ikifuatiwa na Nigeria wenye alama mbili huku Taifa Stars ikiwa na alama moja na hivyo inahitaji kuifunga Misri ili kufufua matumaini ya kufuzu kwa fainali hizo za AFCON.
Taifa Stars itamaliza mechi zake za kufuzu kwa fainali za AFCON 2017 kwa kucheza na Nigeria mwezi September mwaka huu mjini Abuja.
CHANZO:TBC
No comments