Kiwanda cha sukari Kilombero chasaidia jamii
Kiwanda
cha sukari cha Kilombero kimetumia zaidi ya shilingi milioni 200 katika
ujenzi wa miradi mbalimbali ya kijamii katika nyanja za afya na elimu
katika wilaya za Kilombero na Kilosa mkoani Morogoro
Akikabidhi bweni la wasichana la shule ya sekondari ya
Ruhembe lililojengwa kwa gharama ya shilingi milioni 90, Meneja wa Mfuko
wa kusaidia Jamii wa kiwanda hicho Mary Elizabeth ameitaja miradi
mingine kuwa ni ujenzi wa madarasa katika shule za msingi za Ilunga na
Muungano.
Naye Mkuu wa shule hiyo Johannes Ruekulam amesema bweni hilo lenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 48 litaondoa usumbufu wa kutembea kwa zaidi ya kilomita 40 kila siku kwa wasichana wa shule yake.
Na Fatma Matulanga
25 April 2016
Naye Mkuu wa shule hiyo Johannes Ruekulam amesema bweni hilo lenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 48 litaondoa usumbufu wa kutembea kwa zaidi ya kilomita 40 kila siku kwa wasichana wa shule yake.
Na Fatma Matulanga
25 April 2016
No comments