• Breaking News

    Mtendaji akamatwa kwa kuhujumu zaidi ya shilingi milioni 95


    Mtendaji wa Kata ya GILAY LUMBWA iliyopo katika wilaya ya LONGIDO mkoani ARUSHA, PAULO LUCAS anashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kuhujumu fedha
    Mkuu wa Mkoa wa ARUSHA, MRISHO GAMBO
    Mtendaji  wa  Kata  ya  GILAY LUMBWA iliyopo katika wilaya ya LONGIDO mkoani ARUSHA, PAULO LUCAS  anashikiliwa na jeshi la polisi kwa  tuhuma  za  kuhujumu  fedha  zaidi  ya Milioni  95  zilizochangwa  na  wananchi  kwa  ajili  ya  ujenzi  wa shule  ya sekondari ya FILAMINGO ikiwa ni pamoja na vyumba vya  madarasa, maabara na mabweni ya wanafunzi.
    Hatua  hiyo  imefikiwa  baada ya  taarifa  iliyosomwa  na  mkuu   wa  shule hiyo  kuonyesha  kiasi  kidogo cha fedha ikilinganishwa na fedha zilichochangwa  na  wananchi huku Wananchi nao wakidai wamechanga mifugo na fedha taslimu hivyo taarifa hiyo siyo sahihi jambo ambalo Mkuu wa Mkoa wa ARUSHA, MRISHO GAMBO alitaka kupewa taarifa na Mkaguzi wa ndani wa Halimashauri hiyo ndipo ubadhilifu ukabainika.
    Mkurugenzi wa Halimashauri hiyo JUMA MHINA,amesema amepokea taarifa ya Mkaguzi wa ndani inayo onyesha ubadhilifu wafedha katika ujenzi wa shule hivyo Mtendaji huyo hanabudi kuwa mikononi mwa Polisi akisubiri kufunguliwa mashitaka kwa kosa hilo

    No comments

    Post Top Ad