Fahirisi DSE yapungua
Fahirisi
za sekta ya viwanda katika soko la hisa la Dar Es Salaam, DSE
zimepungua kwa alama 2.72 wiki iliyopita kutoka alama 36.26 wiki
iliyotangulia
Meneja Biashara na Masoko wa soko hilo, Patrick Mususa
Meneja Biashara na Masoko wa soko hilo Patrick Mususa
amesema fahirisi hizo zimeshuka kutokana na kushuka kwa bei za hisa za
kampuni ya TOL kwa asilimia 3.61, kampuni ya TCCL kwa asilimia 3.03 na
kampuni ya sigara ya TCC kwa asilimia 0.83.
Ameongeza kuwa fahirisi katika sekta ya huduma za kibenki na fedha pia imeshuka kwa alama 10.36 baada ya hisa ya benki ya CRDB kushuka bei kwa asilimia 1.33.
chanzo:TBC
Ameongeza kuwa fahirisi katika sekta ya huduma za kibenki na fedha pia imeshuka kwa alama 10.36 baada ya hisa ya benki ya CRDB kushuka bei kwa asilimia 1.33.
chanzo:TBC
No comments