Serikali kuboresha TBC
Waziri
wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo NAPE NNAUYE amesema serikali iko
katika mkakati wa kuliboresha Shirika la Utangazaji Tanzania - TBC
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo NAPE NNAUYE
amesema serikali iko katika mkakati wa kuliboresha Shirika la Utangazaji
Tanzania - TBC kwa kulipa uwezo wa ushindani dhidi ya vyombo vya habari
vya ndani na vile vya kimataifa.
Waziri NAPE ameyasema hayo katika mkutano wa pamoja na wadau wa sekta ya habari mkoani KAGERA katika ziara yake ya siku moja mkoani humo.
Waziri NAPE ametoa agizo kwa Halmashauri zote nchini kutoa mamlaka kamili kwa maafisa habari na kuwawezesha kufanya kazi zao kwa ufanisi
Katika mkutano huo baadhi ya maafisa habari kutoka wilaya tano za mkoa wa Kagera wamekabidhiwa vitendea kazi aina ya ipad huku wadau mbalimbali wakitoa ushauri juu ya namna ya kuboresha sekta ya michezo, sanaa na utamaduni pamoja na tasnia ya habari kwa ujumla.
Na Charles Mwebeya
15 April 2016
Waziri NAPE ameyasema hayo katika mkutano wa pamoja na wadau wa sekta ya habari mkoani KAGERA katika ziara yake ya siku moja mkoani humo.
Waziri NAPE ametoa agizo kwa Halmashauri zote nchini kutoa mamlaka kamili kwa maafisa habari na kuwawezesha kufanya kazi zao kwa ufanisi
Katika mkutano huo baadhi ya maafisa habari kutoka wilaya tano za mkoa wa Kagera wamekabidhiwa vitendea kazi aina ya ipad huku wadau mbalimbali wakitoa ushauri juu ya namna ya kuboresha sekta ya michezo, sanaa na utamaduni pamoja na tasnia ya habari kwa ujumla.
Na Charles Mwebeya
15 April 2016
No comments