Sekta binafsi yashauriwa kupendekeza utekelezaji malengo ya milenia
Makamu
wa Rais SAMIA SULUHU HASSAN ameiagiza sekta binafsi nchini kujadili na
kutoa mapendekezo ya namna itakavyoshiriki kwenye utekelezaji wa malengo
mapya ya maendeleo
Makamu wa Rais SAMIA SULUHU HASSAN ameiagiza sekta binafsi
nchini kujadili na kutoa mapendekezo ya namna itakavyoshiriki kwenye
utekelezaji wa malengo mapya ya maendeleo ikiwa ni njia mpya na bora ya
maendeleo kuliko malengo ya awali ya milenia ambayo yalitekelezwa na
kusimamiwa kwa kiasi kikubwa na serikali.
Makamu wa Rais amesema hayo jijini DAR ES SALAAM baada ya kufungua mkutano wa kwanza kwa wafanyabiashara na wadau wa sekta binafsi unaokutana kuangalia watakavyoshirikiana na serikali kufanikisha malengo mapya 17 ya milenia.
Awali katika uwasilishaji wa mada zao mbalimbali za utangulizi mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa - UNDP, ALVARO RODRIGUES pamoja na Afisa Mtendaji mkuu wa taasisi ya biashara ya Afrika RAYMOND MUBAYIWA wamesema wanaamini ushirikiano huo utaiwezesha Tanzania kupiga hatua kiuchumi.
Na Elisha Elia
15 April 2016
Makamu wa Rais amesema hayo jijini DAR ES SALAAM baada ya kufungua mkutano wa kwanza kwa wafanyabiashara na wadau wa sekta binafsi unaokutana kuangalia watakavyoshirikiana na serikali kufanikisha malengo mapya 17 ya milenia.
Awali katika uwasilishaji wa mada zao mbalimbali za utangulizi mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa - UNDP, ALVARO RODRIGUES pamoja na Afisa Mtendaji mkuu wa taasisi ya biashara ya Afrika RAYMOND MUBAYIWA wamesema wanaamini ushirikiano huo utaiwezesha Tanzania kupiga hatua kiuchumi.
Na Elisha Elia
15 April 2016
No comments