• Breaking News

    Picha: Rais Magufuli Alipomtembelea na Kumjulia Hali Mke wake na Wagonjwa wengine Waliolazwa Muhimbili

    Mke wa Rais wa Tanzania John Magufuli, Janeth, amelazwa katika hospitali ya taifa ya Muhimbili. Jana  Ikulu imetoa picha ya Rais Magufuli akimjulia hali katika wodi ya Sewa Haji.

    Taarifa ya ikulu ilisema , alipokuwa anamjulia hali mkewe, pamoja na  balozi na waziri mstaafu wa Tanzania Omar Ramadhan Mapuri, wagonjwa waliolazwa katika wodi ya Sewa Haji walimshukuru kwa hatua zilizochukuliwa na serikali kuboresha hospitali ya taifa ya Muhimbili

    Pia walisema kuwa licha ya kuboreshwa kwa mazingira ya hospitali, wanapata huduma nzuri kutoka kwa madaktari na wauguzi.
    Rais wa Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiongea na mkewe Mama Janeth Magufuli ambaye amelazwa kwenye wodi ya Sewa Haji katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam akipatiwa matibabu jana Novemba 10, 2016. Kulia ni Dkt Edward Ngwale akiwa na wauguzi katika wodi hiyo.
    Rais wa Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimjulia hali Waziri wa Zamani Balozi Omar Ramadhani Mapuri ambaye amelazwa kwenye wodi ya Sewa Haji katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam akipatiwa matibabu jana Novemba 10, 2016.
    Rais wa Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiwashukuru na kuwapongeza kwa kazi nzuri baadhi ya madaktari na wauguzi kwenye wodi ya Sewa Haji katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam alipotembelea wagonjwa pamoja na mkewe ambaye anapatiwa matibabu jana Novemba 10, 2016.
    Rais wa Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiwafariji baadhi ya wagonjwa kwenye wodi ya Sewa Haji katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam alipotembelea kuona wagonjwa pamoja na mkewe ambaye anapatiwa matibabu hapo jana Novemba 10, 2016.

    No comments

    Post Top Ad