• Breaking News

    JPM- NAWASHUKURU KWA KULIOMBEA TAIFA

     

    RAIS John Magufuli amewashukuru viongozi na waumini wa Kanisa la Anglikana na madhehebu mengine, kwa kuendelea kuliombea Taifa na kudumisha amani ma utulivu.

    Alisema hayo jana alipoungana na waumini wa Kanisa la Anglikana la Mtakatifu Albano, Dar es Salaam, kusali ibada ya Jumapili ya kuadhimisha Siku ya Bwana ya 19 baada ya Pentekoste.

    Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Ikulu, Gerson Msigwa, Rais aliongozana na mkewe, Mama Janeth. Alisema Rais wakati akizungumza na waumini wa kanisa hilo baada ya kumalizika kwa Ibada, aliwashukuru viongozi na waumini wote nchini kwa kuendelea kuliombea Taifa.

    Rais Magufuli alisisitiza kuwa viongozi wa dini, wanafanya kazi kubwa na muhimu katika Taifa na kwamba watanzania wote bila kujali dini zao, itikadi za kisiasa, makundi na kada zao, wana wajibu wa kuungana na viongozi hao ili nia hiyo njema iendelee kufanikiwa.

    “Ninawashukuru kwa sababu mnaendelea kuliombea Taifa hili, ninawashukuru kwa sababu siku zote mmekuwa mkipiga magoti na kumtanguliza Mungu mbele, ninawashukuru kwa sababu mnaendelea kuombea amani ya nchi yetu na upendo udumu ndani yetu sisi sote.

    No comments

    Post Top Ad