RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 81 & 82 (Riwaya inawafaa kuanzia miaka 18 na kuendelea )
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA
Nikamfwata
Sheila na kumkumbatia kwa furaha, huku nikimzungusha zungusha hewani na
kumsimamisha chini, huku nikimbusu busu mdomoni mwake"
"Ngoja kwanza, baby nahitaji unijibu swali langu?"
"Uliza tu mke wangu nitakujibu haraka haraka"
Nilizungumza kwa furaha, kwa huku nikilisubiria kwa hamu swali ka mke wangu mtarajiwa Sheila
"PHIDAYA NI NANI YAKO?"
"Eheeee!"
"Hujanisikia nirudie au?"
Sheila alizumgumza, huku akinitazama kwa sura iliyo anza kujikunja kwa hasira kali.
ENDELEA
"Ohhh baby, huu sio muda muafaka wa kulizungumzia hilo, tuzungumze juu ya harusi yetu."
"Eddy nahitaji kulijua hilo, nililo kuuliza"
"Sheila unanipenda?"
"Ndio, ninakupenda ndio maana nilikaa, bila ya kuwa na mwanaume nikikusubiria wewe"
"Ok ninakuomba tuachane na hiyo mada, kinacho paswa ni....."
"Nikujua Phidaya ni nani kwako"
Sheila
alizungumza huku akiwa ame itumbulia mimacho, kwa mbali machozi
yakianza kumlenga lenga. Kitu kilicho anza kunichanfanya ni namna gani
amemjua Phidaya.
"Sipo katika wakati mzuri wa kulizungumzia hilo swala sasa hivi, ninakuomba tuliache"
"Eddy, Eddy, Eddy"
Sheila alizungumza, huku aking'ata meno yake, kwahasira huku machozi yakimtiririka mashavuni mwake.
Akaitoa simu yangu kwenye kipochi chake, akafungua fungua baadhi ya mafaili, na kunigeuzia kwangu.
"Hii ni nini?"
Nikaiona picha ya Phidaya, akiwa na mtoto anaye fanana na mimi, ambaye John, alinibia anaitwa Junio
"Eddy kwa nini, hukua mkweli kwangu, kwa nini uliamua kuzaa na mwanamke mwengine wakati unatambua mimi nipo?"
Sheila
alizungumza huku akiwa ameishika simu yangu, na kunisogezea karibu na
uso wangu ili nimuone mtoto huyo, ambaye kila kitu amefanana na mimi.
Hata mama akimuona hata kua na haja ya kuuliza huyu ni mtoto wa nani.
Nikaikwapua
simu yangu, kutoka mkononi mwa Sheila, na kukaa kitandani huku
nikiendelea kumtazama mwanangu huyu mwenye mvuto wa kila aina.
"Eddy, ni kosa gani nilikufanyia lakini, hadi ukaamua kunisaliti ehee?"
"Au kwasababu mimi ni muafrika, ukaona ukazad na huyo muarabu?"
"Au sikua mwanamke sahahi kwenye maisha yako si ndio?"
Sheila
alizungumza huku akiendelea kulia kwa uchungu, huku akinitazama usoni
mwangu. Kwa upande mmoja, nifaraja kumuona mwanangu japo kwa picha ila
kwa upanfe mwengine imeanza kuniletea uchungu kwani sikuhitaji mtu
yoyote atambue nina mtoto, hadi nitakapo amua mimi kufanya hivyo.
"Eddy si ninazungumza na wewe, lakini?"
"Ninakuomba unyamaze"
"Eddy siwezi kunyamaza, dhamani yangu mimi ipo wapi?"
"Sheila funga bakuli lako, unataka dhamani gani zaidi ya mimi kukuoa wewe, au unataka nimuue huyu mtoto si ndio?"
Nilizumgumza
kwa kufoka huku nikimtazama Sheila, aliye anza kurudi nyuma baada mimi
kunyanyuka kitandani kwa kasi. Sheila alianza kutetemeka, baada ya
kugundua nimekasirika, sana.
"Hii ishu ibaki kuwa mimi na wewe, sihitaji mama atambue sawa?"
"Kwa nini, hutaki ajue?"
"Hilo sio ombi, bali ni amri"
Nilizungumza na kutoka nje, kwenda sehemu ya kupumzikia, ambapo kuna baa kubwa tuu
"Nikusaidi nini?"
Dada muhudumu, alizungumza huku akinitazama machoni
"Una pombe kali?"
"Aina gani?"
"Nipe yoyote, ili mradi iwe pombe kali"
"Nusu glasi, au glasi nzima?"
"Lete mzinga mzima"
Dada huyu akanitazama mara mbili mbili, usoni na kuondoka.
"Hii picha ameitoa wapi huyu mwanamke?"
Nilijiuliza
huku nikiendelea kuitazama picha iliyopo kwenye simu yangu. Nikapata
wazo la kuingia kwenye mtandao wa Whatsappp, ila sikuona picha yoyote
iliyo ingia kupitia mtandao huo. Nikaingia Viber ila sikuona chochote.
Muhudumu akaweka mzinga wa pombe kali mezani
"Usiniwekee glasi wewe nenda nayo"
Muhudumu akaondoka
"Wewe dada, ni bei gani?"
"Huo ni elfu semanini"
Nikatoa
walet mfukoni na kutoa noti kumi za shilingi elfu kumi, nikamakabidhi
muhudumu, akanipa asante na kuondoka. Nikaanza kufakamia mafumba ya
pombe, iliyo ngumu kumeza kooni mwangu, ila muda mwengine, ikanilazimu
kufumba macho ninapo imeza.
Nikiwa
kwenye dimbwi la mawazo, mlio wa simu, yangu ukanistua. Sikujua ni
namba gani inayo piga kwa haraka nikaipokea na kuiweka sikioni
"Eddy umeoa?"
Nisauti
ya Phidaya, ilisikika upande wa pili wa simu, nikajikuta nikipatwa na
kigugumizi cha kulijibu swali hilo, baada ya Sheila kukaa kwenye kiti
cha karibu yangu.
"Ngoja nitakupigia"
Nikakata simu, na kumtazama Sheila aliye kaa mbele yangu.
"Eddy umeanza lini kunywa?"
"Kwani vipi?"
"Nimekuuliza tuu"
"Ninakuja"
Nikanyanyuka
na kumuacha Sheila peke yake mezani, nikaingia chooni na kuipiga namba
aliyo ipiga Phidaya, ikaita kwa muda ikapokelewa
"Wewe nani?"
Nilisikia sauti ya mtoto ikizungumza, nikakaa kimya kusikilizia
"Mama kuna mtu amepiga simu yako, hazungumzi"
Mtoto huyo niliye amini kwamba ni Junio nilimsikia akizungumza
"Haloo"
Nikaisikia sauti ya Phidaya akizungunza

No comments