RIWAYA: She is My Wife- Sehemu ya 35 & 36
Mwandishi: EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA
“Asante sana Fred”
Wakiwa
juu angani, wakaendelea kupata vinywaji mbalimbali, huku wakitazama
baadhi ya chanel, za tv ndogo iliyopo kwenye kila meza ya safa lililopo
ndani ya ndege hiyo ya kifahari. Gafla Rahab akaanza kujihisi vaibaya
vibaya, huku mara kadhaa, akawa anajikaza ili Praygod asijue ni kitu
gani kinacho endelea, ila gafla akajikuta akianza kutapika na kulichafua
gauni lake alilo livaa
ENDELEA
Furaha
ikabadilika na kuwa mshike mshike ndani ya ndege kwani kadri muda
ulivyo zidi kwenda hali ya Rahab ikaanza kubadilika na kujikuta mwili
mzima ukianza kumtetemeka, na kutoa mapuvu mdomoni mwake. Frednando
akawaamuru marubani wairudishe ndege haraka kwenye kiwanja cha nyumba
kwake ili kumuwahisha Rahab, aweze kuonana na madktari.
Macho
ya Rahab yakabadilika na mboni zake nyeusi zikapotea na kubaki weupe
kwenye macho yake jambo lililozidi kumchanganya raisi Praygod pamoja na
Frednando ambaye hakujua ni ugonjwa gani ambao bibi harusi ameweza
kuupata.
Haikuchukua
muda mwingi, matairi ya ndege yakawa yanaserereka kwenye ardhi ya
uwanja wa nyumbani kwa Frednando, ambapo Alisha waeleza madaktari wake
wawe tayari kwa kumpokea mgonjwa.
Kwa
kushirikia na Frednando, wakambeba Rahab na kumtoa nje ya ndege na
kumuingiza kwenye gari maalumu la wagonjwa lililokuwa likiwasubiri. Moja
kwa moja Rahab akakimbizwa kwenye jingo linalo tumiwa na Fredando kama
hospitali inayo mtibu yeye na familia yake pale wanapo patwa, na hali
yoyote ya kuumwa. Uzuri wa eneo lilipo jumba la Frednando, aliweza
kuwekeza pesa nyingi kujijengea vitu muhimu kwa mahitaji yake, ikiwemo
jengo la hospitali, lenye madaktari bingwa ambao Fredinando anawaamini
sana
“Kaka hivi mke wangu atapona kweli?”
Raisi
Praygod alizungumza huku machozi yakimlenga lenga, akamshuhudia mke
wake akipakizwa kwenye kitanda cha matairi baada ya kushushwa ndani ya
gari, na moja kwa moja akaingizwa kwenye chumba kilicho jaa vifaa muhimu
kwa kumuhudumia mgonjwa mahututi
“Atapona tu, usijali rafiki yangu”
Fredinando
alimfariji raisi Praygod, lakini yeye mwenye amechanganyikiwa kwani
hakuamini kama siku kama hiyo kutajitokeza jambo kama hilo la
kuhuzunisha. Wakiwa wamesimama kwenye nje ya mlango wenye kioo kikubwa,
wakawashuhudia madaktari wakitumia mashine za kustulia mapigo ya moyo
wakiziweka kwenye kifua cha rahabu ambaye amezima kabisa mapigo yake ya
moyo.
Machozi taratibu yakaanza kumtoka raisi Praygod, hakuamini uzuri wote wa Rahab, unaweza kupotea muda wowote kuanzia sasa.
“Kaka jikaze”
Frednando
alizungumza huku, naye machozi yakiwa yanamtiririka, uchungu anao upata
rafiki yake, nao unaugusa moyo wake, kwani ni dakika chacha tu wametoka
kucheka na kufurahi na shemeji yake ambaye muda mwingi anapenda
kumtania kwa jina la ‘AFRICAN QUEEN’. Mashine zakupulia zinazo soma
mapigo ya moyo jinsi yanavyo kwenda yakazidi kuwachanganya madaktari
hawa wane, kwani ni mstari mmoja ulio nyooka ndio unakatiza kwenye
mashine hiyo, huku kukisomeka sifuri mbili za rangi nyekundu zikiashiria
kwamba Rahab mapigi ya moyo hayafanyi kazi, moja inawezekana amesha
fariki au moyo wake upepata mstuko mkubwa
***
Si
Fetty wala mwenzake yoyote aliye weza kujinyanyua kutoka kwenye sakafu
walipo kaa, kila mmoja macho yake yaliyo jaa machozi, wakawa wanaitazama
sura ya kipande cha mwanaume, aliye fura kwa hasira na si mwingine bali
ni bwana Rusev, aliye simama huku bastola yake ikiwa mkononi mwake.
Kila mmoja akatamani kujitetea, ila nguvu hakuwa nazo za kutosha kusema
anaweza kupambana na bwana Rusev, anaye onekana kuchukia baada ya
mapiganaji yake matatu kuuliwa kinyama
“Hatuna tulicho kibakisha tena duniani, tumekuwa ni watu waovu. Hatuna pa kwenda zaidi ya kaburini. Tuue sisi yupo tayari”
Anna
alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake, huku mikono yake
yenye kufungwa pingu akiendelea kumshika Halima, aliye kwenye hali ngumu
sana.
“Ehee Mungu zipokee roho zetu, na utusamee makosa yetu tuliyo yafanya. Amen”
Anna
alizungumza kwa sauti ya unyonge iliyo wafanya wezake kuendelea kulia
kwa uchungu, kwani hakuna aliye tarajia kwamba maisha yake yatakuwa
hivyo. Maneno ya Anna, yakamfanya bwana Rusev, kumwagikwa na chozi
lililo washangaza askari wake waliopo nje wakiwatazama.
Bwana
Rusev akawamrisha askari wake kuingia ndani na kuwechukua Fetty na
wezake, ambapo akawaamrisha wavalinye vipande vya vigunia vyuesi kwenye
vichwa vyao wasijue ni wapi wanapelekwa.
No comments