• Breaking News

    Taarifa kutoka Ikulu: Rais Magufuli ateua Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Bima la Taifa (NIC)

    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  tarehe 27 Oktoba, 2016 amemteua Bw. Samwel Peter Kamanga kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Bima la Taifa (NIC).

    Bw. Samwel Peter Kamanga ameteuliwa kushika wadhifa huo kuanzia  tarehe 27 Oktoba, 2016.

    Kabla ya uteuzi huo, Bw. Samwel Peter Kamanga alikuwa akikaimu nafasi hiyo.

    Gerson Msigwa
    Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
    Dar es Salaam

    No comments

    Post Top Ad