lowasa uso kwa uso na magufuli
Leo
Agosti 27, 2016 Rais mstaafu wa awamu ya tatu wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Benjamin Mkapa na mkewe Anna Mkapa wameadhimisha miaka 50 ya
ndoa yao tangu walipooana.
Kikubwa kilichowavutia watu wengi katika maaadhimisho hayo ni kumuona Rais John Pombe Magufuli akiwa na aliyekuwa mpinzani wake wa karibu wakati wa uchaguzi, Edward Lowassa.
Rais
Benjamin Mkapa alikuwa Rais wa Tanzania kuanzia mwaka 1995 hadi 2005
akiwa ndiye Rais wa kwanza tangu kuanza kwa mfumo wa vyama vingi nchini.

