• Breaking News

    ULAJI BROKOLI HUTUEPUSHA NA MAGONJWA HATARI.-UTAFITI.

    Mboga aina ya brokoli












    Ulaji wa mboga aina ya brokoli (broccoli) waweza kupunguza uwezekano wa kupata magonjwa 
    hatari ya moyo, kisukari aina ya pili, pia aina mbalimbali za saratani. Dutu 
    zijulikanazo kama flavonoids katika vyakula hivi, husaidia mwili kuweza kupambana na maradhi hayo
     hatari yanayotishia maisha ya walio wengi.

    Watafiti kutoka chuo kikuu cha Illinois Marekani wanasema kuwa dutu za phenolic ni muhimu katika
     mboga hiyo ya majani  na husaidia
    kuondoa sumu mwilini na kutuepusha na magonjwa mbalimbali.

    Mboga ya majani aina ya kale.









    "Watu walao mboga zenye kiasi kikubwa cha dutu hizo huwa na uwezekano mdogo wa kupata 
    maradhi hayo hatari" anasema Dr Jack Juvik wa kitivo cha sayansi ya vinasaba kutoka 
    chuo hicho. Anaendelea kusema kuwa, " kwa kuwa miili yetu haiwezi kutengeneza dutu hizo,
     hivyo basi ni muhimu kuhakikisha kuwa tunakula vyakula vyenye virutubisho ili kuboresha 
    afya ya miili yetu".

    Utafiti huo unahusisha sayansi ya vinasaba ili kuweza kuzalisha brokoli, kabeji na kale zenye
     kiwango kikubwa cha  virutubisho hivyo bila kuathiri ladha za mboga hizo.

    Dr Juvik anasisitiza kuwa, dutu hizo huwa hazibaki mwilini kwa muda mrefu kwa hiyo 
    tunahitajika kula mboga hizo walau kila baada ya siku tatu au nne ili kupunguza uwezekano
     wa kupata magonjwa ya moyo, saratani, kisukari na maradhi mengineyo yanayotutesa.

    No comments

    Post Top Ad