SIMULIZI: FACEBOOK SEHEMU YA 08
USISAHAU KULIKE PAGE YETU YA FACEBOOK HAPA
ILIPOISHIA
"Narejea shule kesho" kwa msisitizo na tabasamu alijibu Reshmail. Mzee Manyama hakuamini kwani alikuwa akiwaza ni namna gani atamshawishi mwanae aweze tena kurejea shuleni baada ya matatizo yote yaliyojitokeza kwa mchumba wake Adam ambaye hadi wakati huo bado mwili wake ulikuwa haujapatikana wala taarifa yoyote zaidi ya nguo zikiwa na matundu ya risasi na damu."asante sana mwanangu nakupenda sana" mzee Manyama aliongea kwa furaha huku akimkumbatia mwanae.
Tangu kupotea kwa Adam aliyehisiwa kuwa tayari amekufa kulipokelewa kwa hisia tofauti na wananchi huku asilimia kubwa ikiegemea upande wa imani potofu za kishirikina wakihusisha tukio hilo na utajiri alionao Mh. Manyama na uchaguzi uliokuwa mbele yake.
INAENDELEA...
"Wamemtoa mwanangu kafara ili waongeze utajiri,nilimwambia
Adam aoe msukuma mwenzake ona sasa,watoto wa siku hizi wabishi wanajifanya
wanajua sana na elimu yao inawadanganya" mama yake Adam alikuwa analaani
vikali mbele ya mume wake wakiwa ndani ya nyumba yao maeneo ya Igoma kwa
'one-way'
"Usiseme hivyo mama Adam kumbuka sisi ni wakristu,tumwachie Mungu yeye ndio atajua nini cha kufanya" Babaye Adam alimtuliza mkewe huku akimgongagonga mgongoni kwa kutumia kiganja cha mkono wake wa kuume.
Mawasiliano baina ya familia hizi mbili ya Adam jijini Mwanza na ya Reshmail jijini Dar-es-salaam yalikuwa yamekatika licha ya baba yake Adam (mzee Michael) kutangaza kuwa kutoka moyoni mwake amesamehe yote yaliyotokea na anaamini ni mipango ya Mungu lakini kinyongo kilionekana dhahiri kwa matendo,upendo wa zamani haukuwepo tena jambo hilo lilimfadhaisha sana mzee Manyama kiasi cha kukondeana na kukosa umakini katika utendaji wake wa kazi jambo lililoishusha sana heshima yake kama mbunge aliyekuwa anaheshimika sana kuanzia bungeni hadi jimboni kwake,wapinzani walitumia fursa hiyo kumchafua hasahasa na kweli uchafu huo ukakubalika kwa wananchi kwa ujumla Manyama hakuwa na lake tena pale,wananchi walimpuuzia sana tofauti na zamani na hata hiyo miaka miwili iliyobaki wananchi waliiona kama ni mingi sana kuwa na kiongozi wa aina yake.
"Usiseme hivyo mama Adam kumbuka sisi ni wakristu,tumwachie Mungu yeye ndio atajua nini cha kufanya" Babaye Adam alimtuliza mkewe huku akimgongagonga mgongoni kwa kutumia kiganja cha mkono wake wa kuume.
Mawasiliano baina ya familia hizi mbili ya Adam jijini Mwanza na ya Reshmail jijini Dar-es-salaam yalikuwa yamekatika licha ya baba yake Adam (mzee Michael) kutangaza kuwa kutoka moyoni mwake amesamehe yote yaliyotokea na anaamini ni mipango ya Mungu lakini kinyongo kilionekana dhahiri kwa matendo,upendo wa zamani haukuwepo tena jambo hilo lilimfadhaisha sana mzee Manyama kiasi cha kukondeana na kukosa umakini katika utendaji wake wa kazi jambo lililoishusha sana heshima yake kama mbunge aliyekuwa anaheshimika sana kuanzia bungeni hadi jimboni kwake,wapinzani walitumia fursa hiyo kumchafua hasahasa na kweli uchafu huo ukakubalika kwa wananchi kwa ujumla Manyama hakuwa na lake tena pale,wananchi walimpuuzia sana tofauti na zamani na hata hiyo miaka miwili iliyobaki wananchi waliiona kama ni mingi sana kuwa na kiongozi wa aina yake.
Kuliko fedheha yote hiyo Mh. Manyama kwa hiari yake mwenyewe
alipitisha kura ya maoni ya wananchi kuhusu imani waliyonayo kwake kama mbunge
wao. Asilimia 70 ya waliopiga kura walidai hawana imani naye huku asilimia kumi
na nne tu ndio wakidai bado wana imani naye na kura zilizobaki
zikiharibika,rasmi Manyama akawa ametolewa bungeni na katika uchaguzi mdogo
uliofanyika akachaguliwa mbunge kutoka chama cha upinzani na maisha yakaendelea
huku Mh.Manyama akiendelea na biashara zake mikoani.
* **
Adam akiwa pale bustanini alivamiwa ghafla na wanaume wawili wa shoka wakiwa na bunduki,ishara ya kidole mdomoni ilimfanya atulie tuli kisha wakamwonyesha ishara kwamba awafuate alifanya kama walivyotaka hadi kwenye gari iliyokuwa imepaki pembeni kidogo ya nyumba yao Adam alishangazwa sana na ukimya uliokuwepo hakuwepo mlinzi wala mama mkwe wake.Safari yao ilikwenda mpaka Iringa gari iliyokuwa na vioo vyeusi 'tinted' ilimzuia Adam kujua ni wapi alipo,gari ilizimishwa ndani ya jumba kubwa sana ambapo alipelekwa kwenye chumba kikubwa tu,hofu kubwa ilimtawala hakujua kwa nini yuko pale,hakupigwa wala kupewa bughudha yoyote,hali hiyo ilzidi kumshangaza "au ndio wachuna ngozi" alijiuliza Adam kwa hofu tele.
* **
Adam akiwa pale bustanini alivamiwa ghafla na wanaume wawili wa shoka wakiwa na bunduki,ishara ya kidole mdomoni ilimfanya atulie tuli kisha wakamwonyesha ishara kwamba awafuate alifanya kama walivyotaka hadi kwenye gari iliyokuwa imepaki pembeni kidogo ya nyumba yao Adam alishangazwa sana na ukimya uliokuwepo hakuwepo mlinzi wala mama mkwe wake.Safari yao ilikwenda mpaka Iringa gari iliyokuwa na vioo vyeusi 'tinted' ilimzuia Adam kujua ni wapi alipo,gari ilizimishwa ndani ya jumba kubwa sana ambapo alipelekwa kwenye chumba kikubwa tu,hofu kubwa ilimtawala hakujua kwa nini yuko pale,hakupigwa wala kupewa bughudha yoyote,hali hiyo ilzidi kumshangaza "au ndio wachuna ngozi" alijiuliza Adam kwa hofu tele.
Hayo ndio masharti ambayo mama Reshmail alitoa kwa vijana
aliowapa tenda hiyo ya kumtorosha Adam pale nyumbani. Shida yake haikuwa
kumtesa Adam bali kumweka mbali na mwana (Reshmail) ambaye alikuwa
amempagawisha ipasavyo katika mapenzi ya jinsia moja.Suala la pesa halikuwa
tatizo hata kidogo alichohitaji ni kutimiziwa alichotaka. Mkataba wa miaka
mitano ndio alioingia na watu hawa kukaa na Adam bila kumruhusu kutoka nje ya
jingo.Bi Gaudencia aliamini kwamba kwa kutokomea Adam mbele ya uso wa Reshmail
ilikuwa fursa nzuri ya kurudisha tena uhusiano wake na Reshmail ambao ulikuwa
unaelekea kufa lakini kinyume chake alikuwa ameibua chuki kubwa baina yake na
mwanae “heri wote tukose kama ni hivyo” alijiapiza mama Reshmail baada ya
kuona dalili za kumshawishi Reshmail hazipo tena
Alikuwa ni Reshmail
mwingine kabisa mkasa uliomkumba ulimbadilisha sana na kuitanua akili yake
sana,Eveline naye alisikitishwa na yaliyomkumba shoga yake akajitahhdi sana
kuwa karibu naye kumpa moyo huku akijiepusha sana kufanya vitendo ambavyo
vitamkumbusha Resh jinsi alivyoweza kukutana na Adam. Ni katika kujiepusha na
kumkera rafiki yake huyo kipenzi Eveline akajikuta amefuta picha za uchi na
filamu za ngono katika kompyuta yake akawa si mtu wa kutoroka shule,hakuwa tena
mtu wa wanaume na hatimaye akawa Eveline wa kuigwa na wanafunzi wenzake jambo
hilo liliwaduwaza sana wanafunzi pale shuleni lakini ndio hivyo Eve alikuwa
amekubali mabadiliko katika maisha yake. Juhudi zao katika masomo ziliendelea
kuwaweka katika nafasi nzuri ya kufanya vizuri mtihani wao wa mwisho.
Hawakuyazungumzia tena yaliyopita tena walijadili mapya na yanayowanufaisha
"Eveline wewe ni kama dada yangu nakupenda sana"
"Nakupenda pia Reshmail umebadili maisha yangu moja kwa moja nina maisha mazuri sasa" alijibu Eva kwa upole huku akimwangalia Reshmail aliyekuwa anaishusha chandarua yake aweze kulala. Ni kweli walitokea kupendana wawili hawa.
"Hivi Resh una mpango bado wa kusomea uhasibu mi lazima niwe mhasibu"
"Mh! unavyojiaminisha utadhani tumefaulu tayari" alijibu Resh.
"He! mi najua sisi kufaulu kwetu sio swali ni jibu,swali ni je tunaenda chuo gani na kusomea nini." alijiaminisha Eveline.
"ok! nilidhani
nitasomea uhasibu lakini kwa heshima ya Adam nitasomea sheria" alijibu
Reshmail kwa furaha."Nakupenda pia Reshmail umebadili maisha yangu moja kwa moja nina maisha mazuri sasa" alijibu Eva kwa upole huku akimwangalia Reshmail aliyekuwa anaishusha chandarua yake aweze kulala. Ni kweli walitokea kupendana wawili hawa.
"Hivi Resh una mpango bado wa kusomea uhasibu mi lazima niwe mhasibu"
"Mh! unavyojiaminisha utadhani tumefaulu tayari" alijibu Resh.
"He! mi najua sisi kufaulu kwetu sio swali ni jibu,swali ni je tunaenda chuo gani na kusomea nini." alijiaminisha Eveline.
"Mh! na upole wako huo na mambo ya kutoa hukumu wapi na wapi? mwenzio naangalia ankara" alisema Eva.
"Wala hata siendi kuhukumiana naenda kwa heshima tu" alisisitiza Reshmail.
"Mh! haya mheshimiwa hakimu napenda kujitetea kama ifuatavyo" Eve alitania akifuatiwa na kicheko kikubwa kutoka kwa Reshmail.
ITAENDELEA.............................

No comments