• Breaking News

    Jitibu Magonjwa 300 Kwa Kutumia Mti wa Mlonge

    Mlonge au moringa oleifera kwa kiingereza umekuwa ukijulikana kama mti wa miujiza kwa karne nyingi katika baadhi ya nchi za Afrika, Asia na katika nchi za Caribbean. Mti huu umeripotiwa kutibu zaidi ya magonjwa 300 ikiwemo magonjwa mbalimbali sugu.

    Karibu kila sehemu ya mti huu hutumika kama dawa. Majani ya mlonge yanaweza kutafunwa mabichi, yaliyochemshwa kama mboga au yaliyokaushwa na kusagwa kuwa unga. Unga wa mlonge unaweza kuhifadhiwa kwa miezi kadhaa bila kupoteza ubora na faida zake za kiafya.

    Mbegu za mlonge zimekuwa dili kubwa duniani kwa sasa, zinahitajika kwa kiasi kikubwa katika nchi ya Marekani na China na kwa mujibu wa taarifa ni kuwa zinauzwa mpaka 45000 ya Tanzania kwa gramu 500. Walikuja pia wachina kuzinunua kwa wingi na walikuwepo hapa bei ya mbegu za mlonge ilifika mpaka 11000 kwa kg kwa bei ya jumla yaani kwa anayechukua kg 100 au 500 au 1000 na kwenda juu. Taarifa zisizo rasmi zinadai wachinja hawa walikimbia nchini baada ya serikali kuanza kufuatilia na kuwakamata wakwepaji kodi bandarini. Isingekuwa hivi mpaka leo mlonge ungekuwa umeshatowka wote Tanzania.


    Faida za mlonge zimeandikwa na majarida ya afya na lishe kadhaa duniani. Kile ulikuwa hujui ni kuwa viwanda na makampuni mengi ya dawa za hospitalini yamekuwa yakitumia virutubishi vilivyomo kwenye mti huu kutengenezea madawa kwa ajioli ya binadamu na wanyama.

    Mlonge una:

    Kalsiumu mara 17 zaidi ya ile ya maziwa ya ng’ombe

    Potasiamu mara 15 zaidi ya ile ya kwenye ndizi

    Una vitamini A mara 10 zaidi ya ile ya kwenye karoti

    Una protini nyingi mara 9 zaidi ya ile ya kwenye mtindi

    Una klorpfiti (kemikali ya rangi ya kijani ipatikanayo katika mimea) mara 4 zaidi ya ile ya kwenye nyasi au majani ya ngano (wheatgrass)

    Una madini chuma mara 25 zaidi ya yale ya kwenye Spinach

    Una vitamini A mpaka Z

    Una omega 3, 6 na 9

    Una asidi amino zile muhimu zinazohitajika na mwili

    Una kiasi cha kutosha cha madini ya zinc ambayo ni madini muhimu katika kuongeza homoni za kiume na nguvu za kiume kwa ujumla

    Mlonge ndicho chakula chenye afya zaidi juu ya ardhi:

    Mlonge una jumla ya virutubishi 92, mmea au mti mwingine wenye virutubishi vingi basda ya mlonge una virutubishi 28. Mlonge una vionsa suku 46 na viondoa uvimbe mbalimbali mwilini 36, una asidi amino 18 na asidi amino muhimu zaidi 9 ambazo miili yetu haina uwezo wa kuzitengeneza.

    Unga wa majani ya mlonge unao uwezo wa kutibu magonjwa zaidi ya 300 mwilini, magonjwa hayo ni pamoja na :

    1. HUko Afrika magharibi madaktari hutumia mlonge kutibu kisukari.

    2. HUko India mlonge hutumika kutibu shinikizo la juu la damu

    3. HUtibu matatizo u maumivu ya mishipa

    4. Hutuliza mapigo ya juu ya moyo

    5. Hutibu kansa

    6. Pumu

    7. Hutuliza wasiwasi

    8. Kikohozi

    9. Maumivu ya kichwa

    10. Inazuia na kushusha ile lehemu hata ile ya juu zaidi

    11. Inapunguza mafuta tumboni

    12. Inaweza sawa homoni

    13. Inatibu maumivu wakati wa hedhi

    14. Unasafisha ini

    15. Inasafisha mkojo na kibofu cha mkojo

    16. Inarekebisha matatizo kwenye tezi

    17. Unatibu kipindupindu na kuharisha

    18. Kifua kikuu

    19. Kichwa kizito

    20. Uchovu

    21. Mzio

    22. Vidonda vya tumbo

    23. Maambukizi kwenye ngozi

    24. Maumivu mbalimbali mwilini

    25. Huondoa madoa doa meusi kwenye ngozi

    26. Husafisha damu

    27. Hutibu matatizo kwenye koo

    28. Huondoa makohozi mazito kooni

    29. Huondoa taka na msongamano kifuani

    30. Hutibu kipindipindu

    31. Huondoa moto wa jicho au uvimbe kwenye jicho

    32. Hutibu maambukizi kwenye macho na kwenye masikio

    33. Unatibu homa

    34. Maumivu kwenye maungio

    35. Huondoa chunusi

    36. Hutibu matatizo karibu yote ya ngozi na kinga ya mwili

    37. Matatizo kwenye mfumo wa upumuaji

    38. Inatibu kiseyeye

    39. Huongeza uwingi wa mbegu za kiume na nguvu kwa ujumla

    40. Inatibu minyoo

    41. Huongeza maziwa kwa wingi kwa mama anayenyonyesha

    42. Huondoa uvimbe kwenye utumbo mpana

    43. Inatibu ugonjwa wa kuvimba mwili

    44. Inatibu kuhara damu

    45. Inatibu kisonono

    46. Unatibu tatizo la kukosa usingizi

    47. Unatibu homa ya manjano

    48. Unatibu malaria

    49. Unatibu U.T.I na matatizo mengine kwenye mfumo wa mkojo

    50. Unasaidia pia kujenga na kuimarisha misuli

    51. Unatibu magonjwa ya mifupa

    Mlonge uansafisha mwili wako wote, unasafisha ini, figo, moyo, macho, unaimarisha meno, ngozi na nywele. Wakati unatumia mlonge unakufanya ujisikie vizuri, ujisikie mpya na mwenye nguvu. Watu wengi wanaotumia mlonge huwa ni wenye afya nzuri hata kwa muonekano tu hata wanapokuwa na umri mkubwa zaidi ya miaka 90.

    Majani ya mti wa mlonge pia yanaweza kutumika kutengeneza biogas. Hutumika pia kama chakala cha wanyama kama sungura , mbuzi, ng’mbe. Mbwa n.k. Sungura wanaonekana kupenda zaidi mlonge kuliko wanyama wote.

    No comments

    Post Top Ad