Rais MAGUFULI awataka watanzania kumuenzi SOKOINE kwa uadilifu
Rais
Dkt. JOHN MAGUFULI amewataka watanzania kuenzi misingi ya uadilifu
iliyowekwa na aliyekuwa waziri mkuu wa Tanzania HAYATI EDWARD MORINGE
SOKOINE aliyefariki kwa ajali ya gari mwaka 1984.
machache wakati wa Ibada ya Kumbukumbu ya miaka 32 ya Kifo cha
aliyekuwa Waziri Mkuu Hayati Edward Moringe Sokoine katika kanisa la
Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam
Rais MAGUFULI amesema hayo wakati wa ibada ya kumbukumbu ya
miaka 32 ya kifo cha EDWARD MORINGE SOKOINE pamoja na viongozi
mbalimbali wa serikali na Madhehebu ya Dini.
Kwa upande wao Rais Mstaafu wa awamu ya TATU, BENJAMIN MKAPA na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la DSM, MWADHAMA POLYCARP, KARDINALI PENGO wameelezea mchango wa Hayati SOKOINE katika maendeleo ya taifa wakihusisha utendaji wake na jitihada zinazofanywa na serikali ya awamu ya tano katika kuharakisha maendeleo ya taifa.
EDWARD MORINGE SOKOINE alikuwa Waziri Mkuu wa Tanzania kwa vipindi viwili tofauti kati ya mwaka 1977 na 1980 ambapo aliongoza tena kati ya 1983 na 1984 alipofariki dunia akiwa na umri wa miaka 46.
Huko, MOROGORO katika eneo la WAMI DAKAWA ilipotokea ajali iliyosababisha kifo cha hayati EDWARD SOKOINE juhudi za ujenzi wa shule ya kumbukumbu ya SOKOINE zimezidi kufifia kutokana na kutokamilika kwa ujenzi wa shule hiyo.
April 13, 2016
MBOZI KATALA
Kwa upande wao Rais Mstaafu wa awamu ya TATU, BENJAMIN MKAPA na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la DSM, MWADHAMA POLYCARP, KARDINALI PENGO wameelezea mchango wa Hayati SOKOINE katika maendeleo ya taifa wakihusisha utendaji wake na jitihada zinazofanywa na serikali ya awamu ya tano katika kuharakisha maendeleo ya taifa.
EDWARD MORINGE SOKOINE alikuwa Waziri Mkuu wa Tanzania kwa vipindi viwili tofauti kati ya mwaka 1977 na 1980 ambapo aliongoza tena kati ya 1983 na 1984 alipofariki dunia akiwa na umri wa miaka 46.
Huko, MOROGORO katika eneo la WAMI DAKAWA ilipotokea ajali iliyosababisha kifo cha hayati EDWARD SOKOINE juhudi za ujenzi wa shule ya kumbukumbu ya SOKOINE zimezidi kufifia kutokana na kutokamilika kwa ujenzi wa shule hiyo.
April 13, 2016
MBOZI KATALA
No comments