Rais Magufuli Atoa Somo Kwa Waandishi wa Habari..Awaomba Waitangaze Tanzania..Majirani Waache Kutangaza Maliasili za Tanzania Kuwa ni zao

Dkt. Magufuli amesema kuwa kama waandishi wasipoitangaza Tanzania hakuna mwingine wa kuweza kufanya hivyo na ndio maana hata nchi jirani wanadiriki kunadi maliasili za Tanzania kuwa zinapatikana nchini kwao.
Aidha rais Magufuli amewaomba wahariri wa habari kuweka kurasa za mbele habari za maendeleo pia sio kila baya ndio ziwe katika ukurasa wa mbele bila kujali mazuri yaliyofanyika kwa wakati huo.
“Kwa ndugu zangu waandishi ninawaomba muitangaze Tanzania, muitangaze Tanzania mmuipende Tanzania, tusiwe wepesi wa kuandika mabaya tu ya Tanzania kila baya lipo kwenye front page zuri hakuna”Rais Magufuli alisema
Bonyeza HAPA
kudownload application ya UDAKU SPECIAL kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
WEKA MAONI YAKO HAPA CHINI
No comments